NEWS

**Exploring Zanzibar: The Intriguing Isle with a Touch of Merriment.

Image
 Welcome to Zanzibar, an island paradise that appears as though it's been plucked from the pages of a fairy tale. Situated off the coast of Tanzania, Zanzibar offers more than just breathtaking beaches and crystal-clear waters. It's a place where history, enigma, and a touch of whimsy converge in a tropical concoction. Prepare yourself as we delve into some entertaining, enigmatic, and downright eccentric facts about this captivating destination! 1. The Spice Island: Beyond Aroma Zanzibar is commonly referred to as the "Spice Island"due to its extensive history of spice cultivation. However, did you realize that the island’s spice trade has resulted in some culinary peculiarities? For example, locals have been known to incorporate cloves into their coffee—yes, cloves! While it may sound peculiar, it provides an aromatic punch that could potentially convert you into a spice aficionado. Just refrain from requesting a clove-infused latte at your neighborhood cafĂ©—unless ...

Sintofahamu bei ya vifurushi Nape aagiza watoa huduma waitwe kuhojiwa


Waziri wa Mawasiliano Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape amesema wizara yake imeiagiza Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) kuwaita watoa huduma baada ya kutokea sintofahamu ya bei ya vifurushi.

Spika Dk Tulia Ackson amemtaka Waziri huyo kufafanua uwepo wa utata wa bei katika vifurushi akinukuu taarifa ya mteja aliyetaka kununua kiasi cha GB 1 lakini akapata MB 800, ikiwa ni pungufu ya MB 200 ya mahitaji yake ikilinganishwa na bei iliyotangazwa.

Kuhusu hilo, Nape ameliambia Bunge kuwa kila baada ya miezi mitatu, watoa huduma wanakuwa na uwezo wa kubadili gharama ya vifurushi.

Hata hivyo mabadiliko hayo hutakiwa kuonekana katika ‘menyu’ ikionesha kiwango na gharama.

Kilichotokea, kwa mujibu wa Waziri, ni kwamba mtoa huduma hakuhuisha taarifa katika bango [menyu].

Wizara imeiagiza TCRA iwaite watoa huduma juu ya suala hilo, ameongeza Waziri.

Suala la vifurushi limeibuka bungeni, Dodoma leo wakati Mbunge wa Mkalama, Francis Mtinga akichangia hoja katika mapendekezo ya Mwongozo wa maandalizi ya mpango na bajeti ya Serikali na mapendekezo ya Mpango Wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka 2023/24.

Mbunge huyo amehoji ikiwa sheria inaweza kutungwa ya kuwabana watoa huduma ya mawasiliano juu ya ukomo wa muda kwa vifurushi akihusisha na ‘wizi’.

Nape aliomba mwongozo kwa lengo la kutoa ufafanuzi na Spika alipompa fursa hiyo akasema: “Bando ni huduma ya ziada.”

Amesema ipo njia ya bila kununua vifurushi ambavyo havina ukomo wa muda ambavyo vinapatikana kupitia “main tariffs.”

Amesema vifurushi ni suala la kibiashara na si la kisheria  huku akisisitiza “nadhani kushutumu ni kuharibu..”

Comments

Popular posts from this blog

"Whispers of the Savannah: The Enchanting Life of Tanzania's Hadzabe Tribe"

Hatua za kufuata unapopoteza kitambulisho cha Taifa

The Secret Guardians of Tanzania's Wild: Unearthing the Myths of Hidden Trolls