NEWS

**Exploring Zanzibar: The Intriguing Isle with a Touch of Merriment.

Image
 Welcome to Zanzibar, an island paradise that appears as though it's been plucked from the pages of a fairy tale. Situated off the coast of Tanzania, Zanzibar offers more than just breathtaking beaches and crystal-clear waters. It's a place where history, enigma, and a touch of whimsy converge in a tropical concoction. Prepare yourself as we delve into some entertaining, enigmatic, and downright eccentric facts about this captivating destination! 1. The Spice Island: Beyond Aroma Zanzibar is commonly referred to as the "Spice Island"due to its extensive history of spice cultivation. However, did you realize that the island’s spice trade has resulted in some culinary peculiarities? For example, locals have been known to incorporate cloves into their coffee—yes, cloves! While it may sound peculiar, it provides an aromatic punch that could potentially convert you into a spice aficionado. Just refrain from requesting a clove-infused latte at your neighborhood cafĂ©—unless ...

Tundu lissu kufanyiwa upasuaji wa 19

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu Machi 14,2018 atafanyiwa upasuaji wa 19 katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven nchini Ubelgiji. 

Upasuaji huo ni mwendelezo wa ambazo amekuwa akifanyiwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikokuwa amelazwa baada ya kushambuliwa kwa risasi akiwa katika makazi yake mjini Dodoma Septemba 7,2017. 

Alipatiwa huduma za awali katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma. 

Taarifa ya Lissu aliyoitoa jana usiku Machi 10,2018 akielezea afya yake amesema licha ya sasa kuweza kusimama bila msaada, amejuzwa na timu ya madaktari wanaomtibu kuwa kasi ya mfupa wa juu ya goti kuunga ni ndogo. 

"Madaktari wangu wamesema wasipoingilia kati na kurekebisha mfupa huo itachukua muda mrefu sana kuunga," amesema. 

Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) amesema madaktari wamemweleza hata mfupa huo ukiunga baada ya muda mrefu, hautaunga kwa namna utakaoondoa hatari ya kuvunjika baadaye. 

"Kwa sababu hizi, madaktari wangu wamependekeza kufanya operesheni nyingine kwenye mfupa wa juu ya goti la kulia Machi 14,2018, nitarudi Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven, Gasthuisberg, kwa ajili ya kufanyiwa operesheni hiyo," amesema. 

Amesema yuko katika mikono salama ya kitabibu chini ya madaktari Profesa Stefa Nijs na Profesa Willem-Jan Mertsemakers ambao amesema ni madaktari bingwa wa mifupa wanaosifika barani Ulaya. 

"Hivyo, msiwe na hofu. Mungu wetu aliyeniwezesha kuwa hai sasa, ataendelea kutenda miujiza kupitia kwa madaktari bingwa hawa," amesema. 

Lissu amesema ataendelea kutoa taarifa za maendeleo ya afya yake kwa kadri itakavyohitajika akiwaomba Watanzania kumuunga mkono yeye na familia yake katika kipindi anachopitia. 

Lissu yupo Ubelgiji tangu Januari 6,2018 alikopelekwa akitokea Hospitali ya Nairobi, Kenya.

Comments

Popular posts from this blog

"Whispers of the Savannah: The Enchanting Life of Tanzania's Hadzabe Tribe"

Hatua za kufuata unapopoteza kitambulisho cha Taifa

The Secret Guardians of Tanzania's Wild: Unearthing the Myths of Hidden Trolls